![]() |
| Strika mahiri wa timu ya Brazil Naymer Junior |
Michuano ya Kombe la Dunia itafanyika nchini Brazil Juni 12,2014. Kama kawaida mastrika wa timu zitakazoshiriki fainali hizo watakwenda kupambana kwa dhamira moja ya kuonyesha uhodari wa kutikisa nyavu na kuinyakua tuzo hiyo binafsi.Kwenye orodha ya Mastraika mahiri ni pamoja na Mario Balotelli wa Italia, Robin van Persie wa Uholanzi na Karim Benzema wa Ufaransa na wakali hao watakuwa kwenye vita hiyo kali kumsaka bingwa wa Kiatu cha Dhahabu kwenye Kombe la Dunia.
Lionel Messi
Mambo hayakuwa mazuri msimu uliopita kwenye kikosi
cha Barcelona, lakini siku zote Lionel Messi hafundishwi kufunga.
Anazijua nyavu vizuri sana na kwamba ndiye atakayeongoza mashambulizi ya
Argentina kwenye fainali hizo za Kombe la Dunia za Brazil.
Kwenye kundi lao, Argentina ipo pamoja na timu za
Bosnia-Herzegovina, Iran na Nigeria na timu hizo hazionekani kuwa ngumu
kiasi cha kumzuia Messi asifunge. Kuna hatari kubwa kwamba huenda Messi
akamaliza vita yake ya kuwania Kiatu cha Dhahabu kwenye mechi hizo za
hatua ya makundi pekee.Sergio Aguero
Aguero ni aina ya washambuliaji ambaye timu nyingi zingependa kuwa na
huduma yake uwanjani. Staa huyo alifunga mabao 28 katika mechi 34
alizochezea mabingwa wa Ligi Kuu England, Manchester City.
Hivyo kama straika huyo ataendelea kuwa kwenye
kiwango hicho kwa mechi zote kwenye fainali hizo za Kombe la Dunia, huku
kikosini Argentina akiwa na uhakika wa kupata pasi za mwisho kutoka kwa
Lionel Messi na Angel Di Maria, hilo litamweka kwenye nafasi nzuri ya
kufunga mabao mengi.
Neymar
Katika klabu ya Barcelona umekumbana na
nyakati ngumu na kushindwa kuonyesha makali yake halisi, lakini
kwenye Kombe la Dunia, Neymar atakuwa na kitu tofauti cha kukifanya
ndani ya uwanja.
Staa huyo anapewa nafasi kubwa ya kulibeba taifa
la Brazil ambalo ni wenyeji wa fainali hizo na alianza kuonyesha makali
yake ya kutikisa nyavu kwenye mchezo wa kirafiki wa ushindi wa mabao 4-0
dhidi ya Panama.
Kama Brazil ya Luiz Felipe Scolari itakuwa kwenye
ubora wake na Neymar akawa staa wao kwenye safu ya ushambuliaji, fowadi
huyo mwenye umri wa miaka 22 ana nafasi kubwa ya kuwa mshindani wa kweli
kwenye vita hiyo ya kuwania Kiatu cha Dhahabu.
Luis suarez
Said PiePie, Nairobi
Luis suarez
Luis Suarez alitajwa kuwa mshambuliaji hatari zaidi barani Ulaya
kwa msimu uliopita, lakini kwenye Kombe la Dunia kwa sasa anapambana na
muda kupona maumivu yake baada ya kufanyiwa upasuaji wa goti mwezi
uliopita.
Lakini, kama atacheza fainali hizo basi bila shaka
mabao yatamfuata na Uruguay itakuwa kwenye nafasi nzuri zaidi ya
kufanya vizuri. Kwenye fainali zilizopita za Kombe la Dunia
zilizofanyika Afrika Kusini, Uruguay ilikomea nusu fainali, lakini mwaka
huu kama Suarez atakuwa fiti na kuongoza safu ya ushambuliaji sambamba
na Edinson Cavani, basi mabingwa hao wa Amerika Kusini watatamba na
Suarez atatimiza ndoto zake.
Cristiano Ronaldo
Staa huyu wa Real Madrid atakwenda kwenye fainali
hizo akiwa kwenye kiwango safi akitokea kutwaa ubingwa wa Ligi ya
Mabingwa Ulaya na kuweka pia rekodi ya mabao.
Fowadi huyo alifunga mabao 51 katika mechi 47 za
michuano yote aliyocheza klabuni Real Madrid kwa msimu wa 2013-14. Huku
akiwa mshindi wa Tuzo ya Fifa ya Ballon d’Or, Ronaldo ndiye anayebeba
matumaini ya Ureno katika fainali hizo za Kombe la Dunia, hivyo ni
lazima afunge mabao kuibeba timu hiyo.
Kama hilo la kufunga mabao atalifanya vizuri basi
moja kwa moja atakuwa ameingia kwenye kinyang’anyiro cha kukinyakua
Kiatu cha Dhahabu cha Fifa kwenye Kombe la Dunia.
Said PiePie, Nairobi

No comments:
Post a Comment